Tuesday, May 1, 2012
MAKAMU WA RAIS DR BILALI AKITEMA CHE CHE BABATI
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania dr Mohamedi Ghalib Bilal amesema umefika wakati kwa serikali kusimamia kidete suala la kuimarisha na kukuza elimu ya ufundi stadi ili kuwajengea uwezo watanzania waweze kukabiliana na soko la ushindani la jumuiya ya afrika ya mashariki ambapo wajasiriamali wameanza kuingia nchini hali ambayo kama serikali italala upo uwezekano watanzania wakawa hawana uamuzi katika kukuza uchumi wao
akihutubia umati mkubwa wa wananchi mjini babati baada ya kuzindua na kutembelea chuo cha VETA amesema umefika wakati kwa serikali kutoa msukumo kwa jamii kujiunga na VETA ili kuleta tija kabla ya sko hilo halijavamiwa na wananchi jirani na Tanzania.
"elimu ya ufundi ni kichocheo cha ajira za mapema kabla ya kukamilika kwa jumuiya ya afrika ya mashariki,lakini idadi ya wanaohitimu ni ndogo mfano takwimu zinaonyesha kuwa 2006 uwiano wa fundi mchundo na mwananchi ni kati ya fundi mmoja 1:1618 halii inatisha kama watanzania wasipoliangalia kwa makini"
Hata hivyo ameitaka serikali kujizatiti kuhakikisha kuwa elimu ya ufundi stadi inakua ili kuongeza pato la uchumi na watanzania wakiwa wanaongoza katika ajira badala ya wageni toka nje ya nchi.
Nae balozi wa Korea ya kusini bw Young Hoon kim amesema serikali yake itahakikisha inaisaidia serikali ya Tanzania ili iweze kupata wataalamu wa teknolojia ya ufundi standi inasimama'
mwisho
akihutubia umati mkubwa wa wananchi mjini babati baada ya kuzindua na kutembelea chuo cha VETA amesema umefika wakati kwa serikali kutoa msukumo kwa jamii kujiunga na VETA ili kuleta tija kabla ya sko hilo halijavamiwa na wananchi jirani na Tanzania.
"elimu ya ufundi ni kichocheo cha ajira za mapema kabla ya kukamilika kwa jumuiya ya afrika ya mashariki,lakini idadi ya wanaohitimu ni ndogo mfano takwimu zinaonyesha kuwa 2006 uwiano wa fundi mchundo na mwananchi ni kati ya fundi mmoja 1:1618 halii inatisha kama watanzania wasipoliangalia kwa makini"
Hata hivyo ameitaka serikali kujizatiti kuhakikisha kuwa elimu ya ufundi stadi inakua ili kuongeza pato la uchumi na watanzania wakiwa wanaongoza katika ajira badala ya wageni toka nje ya nchi.
Nae balozi wa Korea ya kusini bw Young Hoon kim amesema serikali yake itahakikisha inaisaidia serikali ya Tanzania ili iweze kupata wataalamu wa teknolojia ya ufundi standi inasimama'
mwisho
Hii ni ngoma ya jamii ya kabila la wairaq la wagorowa wakifanya vitu vyao baada ya makamu Rais kuwasili kabla ya kuzindua VETA Babati-hawa jamaa ni hatari wasiponyamazishwa ama kufukuzwa eneo la tukio hucheza hata siku tano huku wakiwaalika wenzao jambo ambalo limeonekana kwa maambukizi ya ukimwi ni hatari
MAKAMU Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr Mohamedi Ghalib Bilal akiwasili kwenye eneo la chuo cha Ufundi stadi VETA kilichopo mjini Babati mkoa wa Manyara anaonekana akisalimiana na timu ya wakuu wa wilaya tano za mkoa wa Manyara dakika chache kabla ya kuzindua chu hicho kilichopo eneo la Waang'waray mjini babati leo Aprili 30 mwaka huu-picha na mwandishi wetu wa water pwaa!! pwaa!! pwaa!
Monday, April 30, 2012
Dr BILAL MAKAMU RAIS TANZANIA NDANI YA BABATI VETA
MAKAMU wa Rais Dr Mohamedi Ghalib Bilal leo majira ya saa ya
saa 7 mchana anatarajia kufungua chuo cha ufundi stadi mjini Babati mkoani
Manyara muda mchache baada ya kuwasili kwenye eneo la chuo hicho kilichopo eneo
la Wang’waray.
Lengo la kufunguliwa kwa chuo hicho ni kusogeza elimu ya
ufundi stadi kwa wakazi wa mkoa huo kwa wahunzi na wengineo hususani vijana ambao wengi wao
watapata uwezo wa kujiajiri wenyewe kupitia fani mbalimbali zilizoanza kutolewa
tangu kilipoanza kupokea wanafunzi wapya mwezi Januari mwaka huu.
Aidha kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Manyara Bw Elaston John
Mbwillo amesema dr Bilali kabla ya kuzindua chuo hicho na kupokelewa na waziri
wa elimu na mafunzo ya ufundi bw Shukuru Kawambwa kwa ushirikiano na mkuu wa
mkoa huo atapanda atapanda mti wa kumbukumbu pamoja na balozi wa Korea kusini
walioshirikiana kujenga chuo hicho.
Burudani kedekede zitaburudishwa kwenye eneo la chuo hicho
ili kusherehesha sherehe hizo za ufunguzi kabla ya mkuu wa VETA kumkaribisha
mkuu wa mkoa na hatimaye waziri Kawambwa ambaye atamkaribisha Dr Ghalib kueleza
ujumbe kwa wananchi.
Baadhi ya wananchi wameiambia glob ya water pwaa!! Pwaa!! Pwaa!
Kuwa kuanzishwa kwa chuo hicho ni faraja lakini pia wataweza kuimarisha fani ya
ufundi huo ambayo kwa miaka mingi wamekuwa wakiifanya bila ya ujuzi kamili na kushindwa
kuingia katika soko la ushindani la afrika ya mashariki.
Aidha pia wameitaka VETA kuacha longolongo kwa kuchaguana
kwani kama watatoa uhuru klwa vijana waliomaliza elimu ya msingi bila shaka
wataweza kumsaidia dr JK kukamilisha ndoto zake maisha bora kwa kila mtanzania
sanjari na kutoa ajira kwa zile ajira milioni moja hadi kufikia ukomo wa
uongozi wake.
Subscribe to:
Comments (Atom)
FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE
Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...
-
TAARIFA KWA UMMA Kampuni ya Azam Media Ltd, imebaini vipande vya picha jongefu vinavyosambaa kupitia mitandao ya kijamii vikimuonesha mwigiz...
-
🟡Taarifa za kuaminika ni kuwa Klabu ya Yanga itasafiri Jumatatu hii November 20, 2023 kuelekea nchini Algeria kwa ajili ya mchezo wa kwanza...