Saturday, October 28, 2023
MOSSES PHIRI APEWA RUNGU KUWAUA WAKULIMA WA MPUNGA
Mshambuliajii Moses Phiri leo ana nafasi kubwa ya kuanza kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ihefu Fc ambao utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa saa 1 usiku
Jana katika Mkutano na Wanahabari, Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira alidokeza kuwa kuna wachezaji leo atawapa nafasi ya kuanza. Phiri ni miongoni mwa wachezaji ambao pasipo na shaka, anaweza kutumika kwenye mchezo huo
Ukiacha maoni ya Wanasimba na wale wanaohoji kwa nini Phiri hapewi dakika nyingi za kucheza, katika dakika hizo chache, Phiri ameonyesha kuwa na ufanisi kuliko hata wale wanaoanza
Mijadala imekuwa mingi, leo huenda Wanamsimbazi wakafurahi kwa kumuona Mzambia huyo akianza. Wachezaji wengine ambao wanaweza kutumika leo ni pamoja na Luis Miquissone na Shabani Iddi Chilunda ambaye amekuwa akifanya vizuri katika mechi za kirafiki
**************
MBABE WA YANGA AANDALIWA DOZI YA USINGIZI NA MSHIRIKI WA AFL
Baada ya kikosi cha Simba kurejea kutoka Misri, Meneja wa Habari na Mawasiliano Ahmed Ally alisema nguvu zote zinahamishiwa kwenye mechi zinazofuata katika ligi kuu ya NBC
Mchezo dhidi ya Ihefu Fc ndio unaofuata kwenye ratiba ambapo Jumamosi, Oktoba 28 Simba itashuka uwanja wa Mkapa kumenyana na walima mpunga hao kutoka Mbarali
Ahmed amesema mkakati wa Simba ni kuendelea kugawa vipigo kwa kila timu inayokuja mbele yao. Ahmed amewataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa Jumamosi katika mchezo huo ambao wamedhamiria kutoa adhabu kali kwa ihefu FC
"Sasa focus ni kwenye ligi kuu ya NBC, Tuendelee kugawa dozi kila anaekuja mbele yetu Wana Lunyasi tuanze sasa kujiandaa na mchezo wetu dhidi ya Wababe wao Jumamosi ya October 28 Benjamini Mkapa," alitamba Ahmed
Baada ya mchezo huo, mchezo utakaofuata ni dhidi ya Yanga, utapigwa Novemba 05 katika uwanja wa Benjamin Mkapa.
Pengine huu ndio mchezo ambao mashabiki wa Simba wanausubiri kwa hamu, alama tatu katika mchezo huu zitaendelea kupalilia safari ya ubingwa msimu huu
MKUDE AMGEUKA MO AMDAI FIDIA YA BIL MOJA
Kiungo wa Yanga SC, Jonas Mkude amefungua kesi katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akiidai Kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited (METL) fidia ya Tsh bilioni moja kwa kutumia picha zake katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwemo Instagram na X (zamani Twitter) bila idhini yake.
Mkude ambaye alijiunga na Yanga baada ya kuondoka Simba amefungua kesi ya madai 192 ya mwaka 2023 mbele ya Jaji Butamo Philip dhidi ya kampuni hiyo akidai fidia hiyo Kwa kuvunja haki yake ya msingi.
<
A midfielder of Young SC, Jonas Mkude has opened a case in the High Court in the Dar es Salaam region demanding compensation of one billion Tsh from Mohamed Enterprises Tanzania Limited (METL) for using his photos in various social networks including Instagram and X (formerly Twitter) without his approval.
Mkude, who joined Yanga after leaving Simba, has filed a 192 claim case of 2023 before Judge Butamo Philip against the company claiming compensation for violating his basic right.
<
A midfielder of Young SC, Jonas Mkude has opened a case in the High Court in the Dar es Salaam region demanding compensation of one billion Tsh from Mohamed Enterprises Tanzania Limited (METL) for using his photos in various social networks including Instagram and X (formerly Twitter) without his approval.
Mkude, who joined Yanga after leaving Simba, has filed a 192 claim case of 2023 before Judge Butamo Philip against the company claiming compensation for violating his basic right.
Subscribe to:
Comments (Atom)
FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE
Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...
-
TAARIFA KWA UMMA Kampuni ya Azam Media Ltd, imebaini vipande vya picha jongefu vinavyosambaa kupitia mitandao ya kijamii vikimuonesha mwigiz...
-
🟡Taarifa za kuaminika ni kuwa Klabu ya Yanga itasafiri Jumatatu hii November 20, 2023 kuelekea nchini Algeria kwa ajili ya mchezo wa kwanza...


