Friday, November 19, 2010

18 students are in lock-up in Manyara,breaking news!!

Polisi mkoani Manyara inawashikilia wanafunzi 18 wa shule ya sekondari ya bweni ya Balangdalalu wilayani Hanang mkoani Manyara kutokana na tuhuma za kumshambulia mkuu wa shule hiyo Bw Godlivin Tiaso kwa vitu vyenye ncha kali na mawe na kumsababisia kulazwa kuharibu mali za shule hiyo kutokana na kile kinachodaiwa kumtuhumu kukutwa na mwanafunzi wa kike nyakati za usiku.
akithibitisha kutokea kwa vurugu hizo juzi kamanda wa polisi mkoani Manyara Bw Parmena Sumary akizungumzia tukio hilo (leo Nov 19)amesema polisi imelazimika kuwashikilia wanafunzi hao na kuendelea kuwahoji na wakibainika kuhusika moja kwa moja itawafikisha mahakamani kujibu tuhuma hizo za uharibifu wa mali pamoja na shambulio.
Aidha kamanda Sumary amesema kabla ya wanafunzi hao kumshambulia mkuu huyo wa shule katika tukio hilo lililotokea usiku wa manane walimwandaa mwanafunzi wa kike wa kidato cha tatu kwenda kumwamsha mkuu huyo bw Tiaso ili kumsikiliza matatizo yake na alipotoka nyumbani kwake ,mwanafunzi huyo alimwita pembeni na kutoa ishara kwa wananfunzi wenzake.
Hata hivyo kamanda Sumary amesema wanafunzi hao walianza kumpiga kwa vitu vigumu na mawe wakimtuhumu kumfumania mwalimu na mwanafunzi huyo tuhuma ambazo amesema polisi inazifanyia kazi na kuharibu mali za shule ambazo gharama yake bado haijafahamika.
Kwa upande mwingine mkuu wa shule hiyo Bw Godliving Tiaso alipoulizwa na radio one kwa njia ya simu toka katika hospitali ya Tumaini ya halmashauri ya wilaya ya Hanang alipolazwa amesema tukio hilo limetokana na ukosefu wa nidhamu ya shule lakini pia hakufumaniwa na mwanafunzi huyo kama wananfunzi hao walivyosambaza uvumi huo.
je, wananchi katika hili mnalziungumziaje?
mwisho

wazee wa nchi

FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE

Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...