Monday, April 30, 2012

Dr BILAL MAKAMU RAIS TANZANIA NDANI YA BABATI VETA


MAKAMU wa Rais Dr Mohamedi Ghalib Bilal leo majira ya saa ya saa 7 mchana anatarajia kufungua chuo cha ufundi stadi mjini Babati mkoani Manyara muda mchache baada ya kuwasili kwenye eneo la chuo hicho kilichopo eneo la Wang’waray.
Lengo la kufunguliwa kwa chuo hicho ni kusogeza elimu ya ufundi stadi kwa wakazi wa mkoa huo kwa wahunzi na wengineo  hususani vijana ambao wengi wao watapata uwezo wa kujiajiri wenyewe kupitia fani mbalimbali zilizoanza kutolewa tangu kilipoanza kupokea wanafunzi wapya mwezi Januari mwaka huu.
Aidha kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Manyara Bw Elaston John Mbwillo amesema dr Bilali kabla ya kuzindua chuo hicho na kupokelewa na waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi bw Shukuru Kawambwa kwa ushirikiano na mkuu wa mkoa huo atapanda atapanda mti wa kumbukumbu pamoja na balozi wa Korea kusini walioshirikiana kujenga chuo hicho.
Burudani kedekede zitaburudishwa kwenye eneo la chuo hicho ili kusherehesha sherehe hizo za ufunguzi kabla ya mkuu wa VETA kumkaribisha mkuu wa mkoa na hatimaye waziri Kawambwa ambaye atamkaribisha Dr Ghalib kueleza ujumbe kwa wananchi.
Baadhi ya wananchi wameiambia glob ya water pwaa!! Pwaa!! Pwaa! Kuwa kuanzishwa kwa chuo hicho ni faraja lakini pia wataweza kuimarisha fani ya ufundi huo ambayo kwa miaka mingi wamekuwa wakiifanya bila ya ujuzi kamili na kushindwa kuingia katika soko la ushindani la afrika ya mashariki.
Aidha pia wameitaka VETA kuacha longolongo kwa kuchaguana kwani kama watatoa uhuru klwa vijana waliomaliza elimu ya msingi bila shaka wataweza kumsaidia dr JK kukamilisha ndoto zake maisha bora kwa kila mtanzania sanjari na kutoa ajira kwa zile ajira milioni moja hadi kufikia ukomo wa uongozi wake.

No comments:

FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE

Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...