Tuesday, May 1, 2012

SHEREHE ZA MEI MOSI UWANJA KWARAA BABATI


INGAWA hakuzunngumzia kabisa suala la upandaji wa miti linalosimamiwa na ofisi yake,makamu Rais aliamua kupanda mti baada ya kuzindua chuo cha VETA mkoani Amanyara

Mkuu wa mkoa wa Manyara bw Elaston Mwbillo kushoto akionekana ktaka kummegea ishu makamu wa Rais dr Mohamedi Bilal kulia ni balozi wa Korea Kusini bw Young Hoom kulia

MAKAMU WA RAIS DR BILALI AKITEMA CHE CHE BABATI

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania dr Mohamedi Ghalib Bilal amesema umefika wakati kwa serikali kusimamia kidete suala la kuimarisha na kukuza elimu ya ufundi stadi ili kuwajengea uwezo watanzania waweze kukabiliana na soko la ushindani la jumuiya ya afrika ya mashariki ambapo wajasiriamali wameanza kuingia nchini hali ambayo kama serikali italala upo uwezekano watanzania wakawa hawana uamuzi katika kukuza uchumi wao
akihutubia umati mkubwa wa wananchi mjini babati baada ya kuzindua na kutembelea chuo cha VETA amesema umefika wakati kwa serikali kutoa msukumo kwa jamii kujiunga na VETA ili kuleta tija kabla ya sko hilo halijavamiwa na wananchi jirani na Tanzania.
"elimu ya ufundi ni kichocheo cha ajira za mapema kabla ya kukamilika kwa jumuiya ya afrika ya mashariki,lakini idadi ya wanaohitimu ni ndogo mfano takwimu zinaonyesha kuwa 2006 uwiano wa fundi mchundo na mwananchi ni kati ya fundi mmoja 1:1618 halii inatisha kama watanzania wasipoliangalia kwa makini"
Hata hivyo ameitaka serikali kujizatiti kuhakikisha kuwa elimu ya ufundi stadi inakua ili kuongeza pato la uchumi na watanzania wakiwa wanaongoza katika ajira badala ya wageni toka nje ya nchi.
Nae balozi wa Korea ya kusini bw Young Hoon kim amesema serikali yake itahakikisha inaisaidia serikali ya Tanzania ili iweze kupata wataalamu wa teknolojia ya ufundi standi inasimama'
mwisho










Hii ni ngoma ya jamii ya kabila la wairaq la wagorowa wakifanya vitu vyao baada ya makamu Rais kuwasili kabla ya kuzindua VETA Babati-hawa jamaa ni hatari wasiponyamazishwa ama kufukuzwa eneo la tukio hucheza hata siku tano huku wakiwaalika wenzao jambo ambalo limeonekana kwa maambukizi ya ukimwi ni hatari

MAKAMU Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr Mohamedi Ghalib Bilal akiwasili kwenye eneo la chuo cha Ufundi stadi VETA kilichopo mjini Babati mkoa wa Manyara anaonekana akisalimiana na timu ya wakuu wa wilaya tano za mkoa wa Manyara dakika chache kabla ya kuzindua chu hicho kilichopo eneo la Waang'waray mjini babati leo Aprili 30 mwaka huu-picha na mwandishi wetu wa water pwaa!! pwaa!! pwaa!

Monday, April 30, 2012

Dr BILAL MAKAMU RAIS TANZANIA NDANI YA BABATI VETA


MAKAMU wa Rais Dr Mohamedi Ghalib Bilal leo majira ya saa ya saa 7 mchana anatarajia kufungua chuo cha ufundi stadi mjini Babati mkoani Manyara muda mchache baada ya kuwasili kwenye eneo la chuo hicho kilichopo eneo la Wang’waray.
Lengo la kufunguliwa kwa chuo hicho ni kusogeza elimu ya ufundi stadi kwa wakazi wa mkoa huo kwa wahunzi na wengineo  hususani vijana ambao wengi wao watapata uwezo wa kujiajiri wenyewe kupitia fani mbalimbali zilizoanza kutolewa tangu kilipoanza kupokea wanafunzi wapya mwezi Januari mwaka huu.
Aidha kwa mujibu wa mkuu wa mkoa wa Manyara Bw Elaston John Mbwillo amesema dr Bilali kabla ya kuzindua chuo hicho na kupokelewa na waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi bw Shukuru Kawambwa kwa ushirikiano na mkuu wa mkoa huo atapanda atapanda mti wa kumbukumbu pamoja na balozi wa Korea kusini walioshirikiana kujenga chuo hicho.
Burudani kedekede zitaburudishwa kwenye eneo la chuo hicho ili kusherehesha sherehe hizo za ufunguzi kabla ya mkuu wa VETA kumkaribisha mkuu wa mkoa na hatimaye waziri Kawambwa ambaye atamkaribisha Dr Ghalib kueleza ujumbe kwa wananchi.
Baadhi ya wananchi wameiambia glob ya water pwaa!! Pwaa!! Pwaa! Kuwa kuanzishwa kwa chuo hicho ni faraja lakini pia wataweza kuimarisha fani ya ufundi huo ambayo kwa miaka mingi wamekuwa wakiifanya bila ya ujuzi kamili na kushindwa kuingia katika soko la ushindani la afrika ya mashariki.
Aidha pia wameitaka VETA kuacha longolongo kwa kuchaguana kwani kama watatoa uhuru klwa vijana waliomaliza elimu ya msingi bila shaka wataweza kumsaidia dr JK kukamilisha ndoto zake maisha bora kwa kila mtanzania sanjari na kutoa ajira kwa zile ajira milioni moja hadi kufikia ukomo wa uongozi wake.

FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE

Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...