Friday, November 17, 2023
BODI YA WAKURUGENZI YA SIMBA YATANGAZA KUWAACHA WACHEZAJI
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Salim Abdallah ‘Try Again’ ameweka wazi kuwa wachezaji ambao hawataonyesha uwezo wao na kujituma uwanjani hawatuvumiliwa hivyo wataachwa.
Try Again amesema katika kipindi cha mwezi mmoja na siku chache kilichobaki kuelekea dirisha dogo la usajili kila mchezaji anapaswa kujituma na kuonyesha uwezo wake la sivyo ataachwa.
Try Again ameongeza kuwa Simba haiwezi kuwa na wachezaji ambao wanalipwa kiasi kikubwa cha pesa na bado wanakaa benchi kutokana viwango kushuka.
“Baada ya matokeo tuliyopata siku za karibuni tumefanya tathimini ili kuona tumekwa wapi na tumegundua wachezaji wengi hawajitumi. Tumewaambia hatuta wavumilia kila mmoja anapaswa kujituma,” amesema Try Again.
Akizungumzia dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa mwezi ujao Try Again amesema “tutasajili lakini kwa mapendekezo ya mwalimu mpya ambaye tutamtangaza karibuni.
“Unajua unaweza kumsajili mchezaji hata kutoka Al Ahly lakini akaja hapa na kocha asimtumie, tutampa jukumu hilo yeye kwakuwa ndiye anajua anataka mchezaji wa aina gani kwenye kikosi chake,” amesema Try Again.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE
Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...
-
TAARIFA KWA UMMA Kampuni ya Azam Media Ltd, imebaini vipande vya picha jongefu vinavyosambaa kupitia mitandao ya kijamii vikimuonesha mwigiz...
-
🟡Taarifa za kuaminika ni kuwa Klabu ya Yanga itasafiri Jumatatu hii November 20, 2023 kuelekea nchini Algeria kwa ajili ya mchezo wa kwanza...

No comments:
Post a Comment