Wednesday, November 1, 2023

HEEE CAF CL INA JAMBO LAKE HEBU CHEKISHIA

Lady and Gentleman This year CAF CL will be on flames πŸ”₯πŸ”₯πŸ”₯. Who will be the most scorer of CAF CL 2023-2024 Aziz Ki πŸ‡§πŸ‡« - > Young Africans Sports Club πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Bouli Jr. πŸ‡¨πŸ‡²-> Wydad Athletic Club - WAC πŸ‡²πŸ‡¦ Clatous Chama πŸ‡ΏπŸ‡²-> Simba SC Tanzania πŸ‡ΉπŸ‡Ώ Fiston Mayele πŸ‡¨πŸ‡©-> Pyramids πŸ‡ͺπŸ‡¬ Lucas Ribeiro πŸ‡§πŸ‡·-> Mamelodi Sundowns FC πŸ‡ΏπŸ‡¦ Mahmoud Kahraba πŸ‡ͺπŸ‡¬-> Al Ahly SC πŸ‡ͺπŸ‡¬ Percy Taus πŸ‡ΏπŸ‡¦-> Al Ahly SC πŸ‡ͺπŸ‡¬ Peter Shalulile πŸ‡³πŸ‡¦-> Mamelodi Sundowns FC πŸ‡ΏπŸ‡¦ Tiago azulΓ£o πŸ‡§πŸ‡·-> Petro de Luanda πŸ‡¦πŸ‡΄

TIKETI ZA DERBY VIP A YA SIMBA NA YANGA NoV 5 ZIMEMALIZIKA

Tuesday, October 31, 2023

THE BRITISH AMBASSADOR MR CONCAR HAS VISITED SIMBA SPORTS CLUB=BALOZI WA UINGEREZA AIYEMBELEA KLABU YA SIMBA

The British Ambassador in the country, David Concar has visited our offices in Masaki Dar es Salaam with the aim of understanding various aspects of the club's operations. Concar has said that he is a good follower of the ball and that is one of the things that made him visit our offices. Concar said Simba is one of the clubs that interest him in the country and he sees it doing better in domestic and foreign championships. "I am happy to visit the Simba club, I am a good follower of football, that's why I came here to share my experience with the leaders of Simba," said Ambassador Concar. The Chairman of the Board of Directors Salim Abdallah 'Try Again' has said that the arrival of Concar has been contributed to what happened in the opening of the African Football League championship two weeks ago because it was a big and historic event. "What happened in the African Football League championship has further publicized Tanzanian football, I know it will not end here, Ambassador Concar will continue with our colleagues and this is a benefit for the country," said Try Again. After meeting the Leaders and speaking with the Journalists, Ambassador Concar attended the team's training at the Mo Simba Arena before greeting the players.
Balozi wa Uingereza nchini, David Concar ametembelea ofisi zetu zilizopo Masaki Dar es Salaam kwa lengo la kufahamu mambo mbalimbali ya uendeshaji wa klabu. Concar amesema yeye ni mfuatiliaji mzuri wa mpira na hilo ni moja ya jambo lililomfanya kutembelea ofisi zetu. Concar amesema Simba ni moja ya klabu ambazo zinamvutia nchini na anaiona ikizidi kufanya vizuri katika michuano ya ndani na nje. “Nimefurahi kutembelea klabu ya Simba, mimi ni mfuatiliaji mzuri wa soka ndio maana nimekuja hapa kubadilishana uzoefu na viongozi wa Simba,” amesema Balozi Concar. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Salim Abdallah ‘Try Again’ amesema ujio wa Concar umechangiwa na kilichotokea katika ufunguzi wa michuano ya African Football League wiki mbili zilizopita kwakuwa lilikuwa tukio kubwa na kihistoria. “Kilichotokea katika michuano ya African Football League kimezidi kulitangaza soka la Tanzania, najua haitaishia hapa Balozi Concar itaendelea kwa wenzetu wengine na hii ni faida kwa nchi,” amesema Try Again. Baada ya kuonana na Viongozi na kuongea na Waandishi wa Habari, Balozi Concar alihudhuria mazoezi ya timu katika Uwanja wa Mo Simba Arena kabla ya kusalimiana na wachezaji.

Monday, October 30, 2023

MO DEWJI AUNDA BARAZA LA USHNDI KLABU BINGWA YA AFRIKA NA UBINGWA LIGI YA NBC

Rais wa heshima wa klabu, Mohamed Dewji ‘Mo’ amefanya uteuzi wa wajumbe 21 wa Baraza la Ushauri wa klabu kwa ajili ya maendeleo. Moja ya majukumu ya Raisi wa heshima ni kuhakikisha Uongozi na Utawala bora unazidi kuboreshwa kila wakati ili kuzidi kusukuma gurudumu la maendeleo ya klabu. Baada ya kushauriana na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi na Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Mo amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Baraza la Ushauri ( Advisory Board) wa klabu. 1. Jaji Thomas Mihayo M/kiti 2. Hassan Dalali-Mjumbe 3. Ismail Aden Rage-Mjumbe 4. Evans Aveva-Mjumbe 5. Faroukh Baghoza 6. Swedi Nkwabi-Mjumbe 7. Azim Dewji-Mjumbe 8. Kassim Dewji-Mjumbe 9. Musleh Al-Ruweh-Mjumbe 10. Mohamed Nassor-Mjumbe 11. Mulamu Ng’ambi-Mjumbe 12. Octavian Mshiu-Mjumbe 13. Prof Mohamed Janabi-Mjumbe 14. Hassan Kipusi-Mjumbe 15. Geofrey Nyange-Mjumbe 16. Gerald Yambi-Mjumbe 17. Moses Kaluwa-Mjumbe 18.Crescentius Magori-Mjumbe 19. Juma Pinto- Mjumbe 20. Mwina Kaduguda-Mjumbe 21. Idd Kajuna-Mjumbe Kazi kubwa ya Baraza hili itakuwa ni kuishauri Bodi juu ya maendeleo ya klabu Uongozi na Utawala bora.

MKURUGENZI WA SHERIA WA YANGA AMLILIA SHABIKI WAO ALIYEADABISHWA KWA KIPIGO DHIDI YA MASHABIKI WA MNYAMA

Mkurugenzi wa sheria wa Yanga amesema kesho klabu ya Yanga itawasilisha rasmi malalamiko yake kwenye mamlaka juu ya kitendo cha mashabiki wa Simba kumpiga shabiki wa Yanga jana kwa Mkapa. "Mpira ni upendo, kwa kitendo hiki cha mashabiki wa Simba kumpiga shabiki wa Yanga kiasi hiki sio utu kabisa, hakuna sababu ya msingi kumshambulia mtu kiasi hiki. Labda niwakumbushe washamba wote walioshiriki unyama huu, Yanga na Simba ni Watani wa jadi sio maadui" "Isije kufika siku hatuwezi kukaa kwa pamoja kama ndugu kwa sababu ya UPUMBAVU kama huu. Naiomba bodi ya ligi @tplboard, TFF @tanfootball na Polisi @policetanzania wachunguze suala hili na hatua kali zichukuliwe" "Klabu itawasilisha malalamiko yake rasmi kesho na tutaomba hatua kali zichukuliwe kwa huu unyama.. Shame on you all who're involved in this incident" "Mwenye kumjua na kuwa na mawasiliano ya huyu (Shabiki wa Yanga aliyepigwa na mashabiki wa Simba) anitumie tafadhali" Licha ya Mkurugenzi huyo kulaani tukio hilo lakini baadhi ya wadau wa Soka wamemshauri kabla ya kutoa tamko alitakiwa kutambua Kiini cha kupigwa dhidi y mashabiki wa timu hiyo ambao hawana historia ya matukio kama hayo tofauti na mashabiki wa Yanga ambao walishamchania mshabiki wa soka Moshi na kuichoma moto.lakini pia mji kasoro bahari Morogoro sambamba na kumpiga shabiki wa Coastal Union jijini Arusha baada kumalizika kwa mikwaju kwenye fainali za FA

AMINI USIAMINI HUYU NI SARAFINA MWIGZAJI MAARUFU ALIETIKISA BONGO

Picha mbili tofauti (zamani na sasa) za Leleti Khumalo mwigizaji toka Afrika Kusini, alizaliwa tarehe 30 Machi 1970 kwa sasa ana umri wa miaka 53. Wengi tunamfahamu kwa jina la Sarafina kutokana na movie maarufu aliyoshiriki ya enzi za ubaguzi wa rangi iliyoitwa SARAFINA! Unakumbuka nini kuhusiana na movie ya Sarafina? Mimi kuna baadhi ya matukio yalinitoa machozi na kunifanya niwachukie sana wabaguzi wote wa rangi
Two different photos (past and present) of Leleti Khumalo, an actress from South Africa, she was born on March 30, 1970 and is currently 53 years old. What do you remember about Sarafina's movie? There are some events that brought tears to my eyes and made me hate all the racists

Sunday, October 29, 2023

HARMONIZE APANIA KUWAPAGAWISHA WAKENYA

Harmonize anapomalizia tamasha zake Uganda, ameandika kupitia ukurasa wake wa Facebook kuwa atakuwa Nairobi, Kenya tarehe 4. Harmonize anatarajiwa kufanya ziara zake za muziki kwenye baadhi ya nchi za Afrika mwezi huu ukiisha na Novemba. Amemaliza Uganda anatarajiwa Kenya na nchi zingine Afrika.
As the musician Harmonize finishes his concerts in Uganda, he has written through his Facebook page that he will be in Nairobi, Kenya on the 4th. Harmonize is expected to make his music tours in some African countries this month ending in November. He has finished Uganda and is expected in Kenya and other countries in Africa.

FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE

Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...