Monday, November 13, 2023

JE KOCHA MPYA WA SIMBA NI HUYU BENCHIKHA MBADALA WA ROBERTINOH?

Klabu ya Simba inatajwa kwamba imeanza mazungumzo na Kocha Abdelhak Benchikha ili aweze kuja kuifundisha timu hiyo, mjadala mkubwa hapa ni mshahara wa Kocha huyu ambaye amefanikiwa kubeba makombe mawili makubwa Afrika, Kombe la Shirikisho Afrika na ubingwa wa Super Cup Kwa mujibu wa tovuti ya 'Transfer Market' Kocha huyu mpaka anaondoka RS Berkane ambayo aliipa ubingwa wa CAFCC 2022 alikuwa akilipwa mshahara wa Tsh.Milioni 53 kwa Mwezi. Akaenda kujiunga na USM Algers ambao nao aliwapa ubingwa CAFCC 2023 na ubingwa wa Super Cup, mpaka anachana na miamba hiyo ya Algeria alikuwa akilipwa mshahara unaofika hadi kufikia Tsh Milioni 80+ Kiufupi Kocha Benchikha ni mwalimu mwenye mafanikio makubwa kwa soka la Afrika ila pia ana thamani kubwa sokoni.Kama Simba SC wakiweza kumchukua Kocha huyu basi hapo ndo tutasema "Mkubwa hufanya mambo makubwa"

No comments:

FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE

Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...