Tuesday, December 5, 2023
Saturday, December 2, 2023
AZAM YAMTOLEA SHIJA UCHOVU YAMBANA KOROMEO
TAARIFA KWA UMMA
Kampuni ya Azam Media Ltd, imebaini vipande vya picha jongefu vinavyosambaa kupitia mitandao ya kijamii vikimuonesha mwigizaji na mtengeneza filamu, Deogratius Shija, akiwatuhunu baadhi ya wafanyakazi wa kampuni yetu kwa vitendo vya rushwa.
Kampuni yetu inamuarifu Shija na umma kwa ujumla kuwa, haivumilii vitendo vya rushwa, udanganyifu na mbinu zozote chafu katika kusaili maudhui kwa ajili ya kuonyeshwa katika chaneli zetu, kadhalika hatupendezwi na tabia ya watengeneza maudhui kutunga shutuma dhidi ya watendaji wetu kwa sababu tu kazi zao hazikupitia kwenye chujio la kupima ubora.
Kwasababu hizo, tunatoa muda wa wiki mbili kwa Deogratias Shija, kuwasilisha ushahidi au vielelezo kuhusu tuhuma alizozitoa kwa Mkurugenzi Mtendaji au kwenye mamlaka za kisheria, TAKUKURU, Film Board, au Jeshi la Polisi, ili kuwezesha hatua stahiki zichukuliwe kwa watuhumiwa wote wanaodaiwa kuihujumu kampuni kwa vitendo vyote kinyume na taratibu za kazi.
Kampuni yetu ina utaratibu maalum wa ndani, ulio wazi na shirikishi katika manunuzi ya filamu na maudhui mengine kutoka kwa wazalishaji binafsi.
Azam Media Ltd inatumia fursa hii kuwaomba wadau wa filamu nchini kufuata njia sahihi zinazokubalika kisheria ikiwemo kutoa taarifa kwa Mkurugenzi Mtendaji, Bodi ya Filamu, Polisi au TAKUKURU pale wanapokuwa na ushahidi wa madai yao badala ya kutumia njia ambazo zinaweza kuleta taharuki na taswira mbaya kwa jamii ndani na nje ya Tanzania.
Imetolewa na Idara ya Mawasiliano kwa Umma
1.12.2023
GAMONDI AMPONDA ALI KAMWE
Kocha Mkuu wa Yanga, Miguel Gamondi, ameeleza kutokubaliana na utaratibu wa kuita mchezaji jina la mchezo, akisisitiza umuhimu wa kuangazia timu nzima akisema “Sikubaliani kabisa na huu utaratibu wa kuita mchezo jina la mchezaji, kwa sababu mchezaji hayupo peke yake wapo timu. Jambo muhimu kwangu ni timu sio mchezaji mmoja, ila naelewa ndio utaratibu wa timu kwa ajili ya kufanya marketing, kuwafanya mashabiki waje uwanjani na kuuelewa zaidi mchezo husika, najua huo ndio utara… See more
Friday, December 1, 2023
SIMBA YAWAUATA MAKHIRIKHRI ALIFAJIRI YA SWALASWALA
Kikosi Cha Simba SC Tanzania cha wachezaji 20 ambacho Disemba Mosi alfajiri kitaondoka nchini kwa ndege maalumu kwenda nchini Botswana ambako kitacheza mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Thursday, November 30, 2023
RAIS WA TFF: TUNATAKA TUUPUMZISHE UWANJA WA BENJAMINI MKAPA SASA
“Miundombinu ni jambo ambalo lilikuwa na changamoto sana ,sasa hivi viwanja mmeona vinapendeza lakini uwanja wa Taifa ni uwanja wa serikali. Sisi tunachoangalia ni kuhakikisha uwanja hatuuzidishii matumizi “
“Ikiwezekana ligi zetu ichezwe mechi ya Simba na Yanga tu ,kuhusu ligi mechi zinazoihusu Simba au Yanga zitachezwa sehemu nyingine ,ila wanapocheza wao wenyewe sawa na hata timu ya Taifa tunataka tuangalie sehemu nyingine ya kucheza ili uwanja upumue “
Rais wa shirikisho la soka Tanzania (TFF ) Wallace Karia akielezea mipango ya kuufanya uwanja wa Taifa (Benjamin Mkapa ) uweze kudumu kwa muda mrefu kwa ubora.
HERSI RAIS WA YANGA AUKWAA UENYEKITI WA ACA BARANI AFRIKA
Klabu ya Young Africans SC inampongeza Rais wake Eng. Hersi Ally Said kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Shirikisho la Vilabu Afrika (Africans Clubs Association).
Subscribe to:
Comments (Atom)
FISTON MAYELE ASHINDWA KUTETEMA KWA PERCY TAU WA AL AHLY,CAF YAMUONA NI BORA KULIKO MAYELE
Mchezaji machachari wa Kimataifa wa Afrika ya Kusini na klabu ya Al Ahly Percy Tau amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi za Ndani Barani...
-
TAARIFA KWA UMMA Kampuni ya Azam Media Ltd, imebaini vipande vya picha jongefu vinavyosambaa kupitia mitandao ya kijamii vikimuonesha mwigiz...
-
🟡Taarifa za kuaminika ni kuwa Klabu ya Yanga itasafiri Jumatatu hii November 20, 2023 kuelekea nchini Algeria kwa ajili ya mchezo wa kwanza...






